Saturday, July 25, 2026
spot_img
HomeKenya NewsBuriani Walibora

Buriani Walibora

Kakamega

Collins Chibole na James Boaz Eshitemi

Kifo cha Prof Ken Waliaula walibora huenda ndilo pigo kubwa Zaidi kuwaikutokea kwa ulingo wa Kiswahili na waenzi wa kazi zake.Hadi kifo chake,Ken Walibora amekuwa mlezi wa wengi katika ulimwengu wa kiswahili.

Kando na waandishi, walimu na wahadhiri wengi ambao walikikumbatia Kiswahili katika maandishi, Walibora aliichangamkia lugha ya Kiswahili pia katika baghwabaghwa za kila siku hususan kama mwanahabari na pia kupitia kampeni za kuimarisha lugha ya Kiswahili.

Prof Ken Walibora

Tuzo tatu mtawalia alizopokea za Jomo Kenyatta literature prize kufuatia vitabu vyake, Ndoto ya Amerika, Kisasi Hapana na Nasikia Sauti ya Mama, zinapeana taswira ya mwandishi aliyeumiliki ulimwengu fulani katika uandishi wa lugha. Marehemu amejipatia sifa kutokana na uandishi wake uliokosha wengi, uchapishaji na uhariri vyote ambavyo alifanya kwingi ikiwa ni pamoja na Kidagaa Kimemwozea

Siku Njema, Ndoto ya Amerika,Kisasi Hapana, Nasikia Sauti ya Mama,Damu Nyeusi, Nizikeni Papa Hapa miongoni mwa nyingine.

JAMES BOAZ ESHITEMI

JAMES BOAZ ESHITEMI

Japoย  kwaย  wengiย ย  yaonekanaย  habari ilaย ย  kwanguย  itasaliaย  jinamiziย ย  manakeย  yanikwepaย  manenoย  mahususi yaย  kumrejeleaย  shujaa, jagina na ย gwijiย  โ€˜munguโ€™ waย  waswahiliย  Kenย  Waliaulaย  almaarufuย  Walibora .

Mwakaย  waย  2005 nikiwa shuleย  yaย  msingiย  yaย  Eshiakhuloย  wilayaniย  Mumiasย  kauntiย  yaย  Kakamegaย  ndipo ilikuwaย  kaskiย  yanguย  yaย  kwanzaย  kusikizaย  habari, mawazoย  naย  ulumbiย  waย  mwandishiย  huyuย  mahiriย  kupitiaย  kwaย  vitabuย  alivyoandika.

Riwaya yaย  Siku Njema ,Ndoto ya Almasi naย  Kufaย  Kuzikanaย  niย  miongoniย  tu mwaย  gangeย  zakeย  zilizonivutiaย  katika shuleย  ya msingiย  kutokanaย  naย  jinsiย  alivyozichambuaย  mwalimuย  Linaย  Akacha, kablaย  yaย  kujiungaย  naย  shuleย  yaย  upili ya Lubinuย  nilikokutanaย  na ย bwanaย  Odaliย  Victorย  aliyenipa motishaย  yaย  kuendeleza ย kukisomaย  kiswahiliย  naย  hataย  kukizungumza.

Japoย  kwaย  mukhtasari kutokanaย ย  naย  kaziย  yake Kenย  Waliboraย  nimewezaย  kufunza lughaย  pana yaย  kiswahili,ย  kufanyaย  katikaย  vituoย  kadha vyaย  utangazaji,kandoย  naย  kuwa mhutubuย ย  katikaย ย  makongamanoย  anuwai hapaย  nchini kenya.

Baadayeย  nilijiungaย  naย  chuo kikuuย  chaย  Masindeย  Muliro kamaย  mwalimuย  waย  lughaย  yaย  kiswahili tokeaย  mwakaย  waย  2013 nilikoichangamkiaย  lughaย  hii aulaย  yaย  Kiswahili. Japoย  kwaย  athariย  zaย  lughaย  mameย  maraย  nyingiย  tulijifungaย ย  kibwebweย  naย  kusalitiย  milaย  zetuย  kwaย  kuiasiย  lughaย  mame.ย  Kiswahiliย  kiliniezeshaย  kuisatiliย  jamaa yanguย  kwaย  kuienziย  kazi yake.ย ย 

Mazishi ya Ken Walibora

Japoย  kwaย  mukhtasari kutokanaย ย  naย  kaziย  yake Kenย  Waliboraย  nimewezaย  kufunza lughaย  pana yaย  kiswahili,ย  kufanyaย  katikaย  vituoย  kadha vyaย  utangazaji,kandoย  naย  kuwa mhutubuย ย  katikaย ย  makongamanoย  anuwai hapaย  nchini kenya. Japoย  kwaย  kumbukizi zakeย  Kenย  Waliboraย  niย  kwambaย  mtiย  mkuu umeangukaย  ilaย  viziki vingali na rotuba linapochomoza shamzi kwa wengi huwafikia mwangaza ila kwa wachache huwafaidi. Kwa wengi hunyaa mvua ila kwa wachache huipata mbegu ya kutia arthini.

Amewaleaย  wanahabariย  chipukiziย  kandoย  na kuvipalilia vipaji chipukiziย  katikaย  Nyanja ย zaย  Kiswahili. Itakumbukwaย  kuwa Profย  Kenย  Waliboraย  amekuwaย  kielelezoย  kwaย  waandishiย  wenzake, wanahabari, Na hataย  walimu kwaย  ujumlaย  bilaย  kuwasaza waenziย  asharafuย  waย  lughaย  panaย  yaย  Kiswahili ย naย  tanzuย  zake.

Prof ย Kenย  Waliboraย  amekuwaย  nguzo muhimu katikaย  tasniaย  nzimaย  ya Kiswahili ย na wapenziย  wake. Inaย  maana Waliboraย  amekuwaย  โ€˜munguโ€™ย  waย  waswahili.

Mazishi ya Ken Walibora

Amewaleaย  wanahabariย  chipukiziย  kandoย  na kuvipalilia vipaji chipukiziย  katikaย  Nyanja ย zaย  Kiswahili. Itakumbukwaย  kuwa Profย  Kenย  Waliboraย  amekuwaย  kielelezoย  kwaย  waandishiย  wenzake, wanahabari, Na hataย  walimu kwaย  ujumlaย  bilaย  kuwasaza waenziย  asharafuย  waย  lughaย  panaย  yaย  Kiswahili ย naย  tanzuย  zake.

Tangia ย lughaย  yaย  Kiswahili ย kufanywaย  linkua franka nchiniย  kenyaย  Profย  Kenย  Waliboraย  amekuwaย  mstariย  waย  mbeleย  katikaย  kukilongaย  Kiswahili ย ย haswa katikaย  miktadhaย  ย tofauti tofauti ikiwemoย  makongamano,ย  katikaย  vyuoย  vikuu,taasisi mbalimbaliย  ikiwemoย  shuleย  zaย  upiliย  naย  zileย  zaย  msingi.

Lughaย  aliyoitumiaย  mwandishiย  Kenย  Waliboraย  katikaย  kaziย  zakeย  ilikuwa lughaย  yaย  kipekeeย  iliyosheheniย  ufundiย  waย  kipekee. Ken ย Waliboraย  piaย  ameichoraย  taswiraย  yaย  matabaka mawili; tabaka la wakwasi naย  lileย  la ย walalahoi.

Walibora ย alitoaย  mtafaruku uliopoย  katikaย  uongoziย  kandoย  naย  kuichoraย  pichaย  kamiliย  inayojitokezaย  waziย  katiย  yaย  walioย  naย  kisomoย  bilaย  ajiraย  na wenye ajira bila kisomo katika ukinzani.ย  Kwaย  kauliย  yangu, mwandishiย  Kenย  Waliboraย ย  lichaย  yaย  kututanguliaย  mbeleย  yaย  hakiย  atasaliaย  katikaย  nyoyoย  zetuย  kamaย  waenziย  waย  lughaย  ya Kiswahili kutokana na vile alivyokua naย  ufundiย  waย  namnaย  yakeย  katikaย  tasniaย  nzimaย  yaย  Kiswahili.ย 

Mchango ย wakoย  utatulazimuย  tukuiteย  hayati. Nani ย anakujuaย  niย  msamiatiย  ambaoย ย  umekulaย  wengiย  naย  hataย  kuwaelekezaย  wengiย  waย  adinasiย  ahera. Siku ย zoteย  umesemaย  chemaย  hakidumu โ€ฆ uru Ken Walibora safiri salama mfahamishe JALALI KUWAย  CHINI WINGU NI SAMAWATIย  KWA ย KULITAZAMA.

COLLINS CHIBOLE

COLLINS CHIBOLE

Nakumbuka nikiwa darasa la nne, babangu aliponitunuku kitabu cha siku njema baada ya kuongoza somo la Kiswahili shule ya msingi ya Eshisenye, ikawa riwaya yangu ya kwanza kuisoma maishani na ukawa mwanzo wa ndoto yangu katika uandishi.

Namtambua Walibora kama aliyechangia pakubwa kufanikiwa kwangu katika lugha ya Kiswahili katika mitihani ya Kitaifa ya KCPE na ya KCSE. Kando na taaluma yangu ya ujasiriamali na fedha, kazi ya walibora ndiyo iliyonisukuma kuandika riwaya yangu ya kwanza ya โ€˜Nyota ya Mamaโ€™ kando na tamthilia ya โ€˜Fumbo la Imaniโ€™.

Walibora ni mwanahabari aliyeumiliki ufundi wa kutamaniwa, mkufunzi na mwandishi aliyeukumbatia ucheshi na ulumbi wa kupigiwa mfano. Si ajabu kwamba , marehemu katika uandishi wake alisisitiza kuwa kila nafsi ni sharti itayaonja mauti, kuna visa si haba vya ubashiri ambavyo vinarejelea kifo chake.

Nilipojiunga na radio MMUST FM mwaka 2013, nilianzisha Makala ya โ€˜Kisiwa cha Lughaโ€™ na moja kwa moja Walibora akawa mlezi wa Makala hayo licha ya shughuli nyingi zilizomsetiri.

Walibora ni mwanahabari aliyeumiliki ufundi wa kutamaniwa, mkufunzi na mwandishi aliyeukumbatia ucheshi na ulumbi wa kupigiwa mfano. Si ajabu kwamba , marehemu katika uandishi wake alisisitiza kuwa kila nafsi ni sharti itayaonja mauti, kuna visa si haba vya ubashiri ambavyo vinarejelea kifo chake.

Kutoka kwa ufukara, kongowea mswahili mhusika mkuu katika riwaya ya siku njema mwishoni analitazama wingu la magharibi na tabasamu la ufanisi, milki ya babake ikiwa chini yake pamoja na binti ย Vumilia tamanio la moyo wake.

Kwa mfano katika riwaya ya siku njema, โ€˜mwili wa Mzee Kazikwisha ulipatikana na mwanawe Msanifu Kombo siku kadhaa baada ya kifo chake. Hakujulikana na wengi kuwa alikuwa Juma Mukosi,msomi wa kutajika, maziko ya juma mukosi yalihudhuriwa na idadi ndogo ya watuโ€™. Mtemi Nasaba Bora katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea alipatikana akiwa ameipa dunia kisogo na mazishi yake kuhudhuriwa na idadi ndogo ya watu. Uandishi wa walibora unasetiri ujumbe wa Tumaini.

Kutoka kwa ufukara, kongowea mswahili mhusika mkuu katika riwaya ya siku njema mwishoni analitazama wingu la magharibi na tabasamu la ufanisi, milki ya babake ikiwa chini yake pamoja na binti ย Vumilia tamanio la moyo wake.

Mto kiberenge katika riwaya ya Kidagaa kimemwozea, licha ya kuwa ulisetiri laana na kutafsiriwa kuwa hatari kwa yeyote ambaye angeyanywa maji yake, Imani na Amani wahusika wakuu baada ya kuyanywa maji yake walitulizwa kiu na hatimae haki yao kupatikana na mmoja wao kupendekezwa hata kuwa mfalme katika jamii hiyo. Mti mkuu ushavunjika ila kupitia kazi zake, atazaa, atalea, atakuza, ataelimisha na kuhamasisha. Rabi ailaze roho yake mahala pema.

Mwisho.

RELATED ARTICLES

Most Popular

Recent Comments