Wednesday, April 15, 2026
spot_img
HomeKenya NewsVisa vya dhuluma dhidi ya watoto vyaongezeka Kakamega

Visa vya dhuluma dhidi ya watoto vyaongezeka Kakamega

Seliphar, Kakamega

Kila siku, kila uchao visa vya dhuluma dhidi ya watoto vinaongezeka katika kaunti ya Kakamega. Ni kipi kinachosababisha visa hizi? Ni hatua gani inayochukuliwa dhidi ya wale wanaotenda unyama huu? Haya ni baadhi tu ya maswali ambayo kupata majibu yake ni muhali.

Hata hivyo wanaskautiย  kutoka katika kaunti ya Kakamegaย  wamejitosa uwanjani kukashifu maovu hayo dhidi ya watoto. Wanaskauti haoย  wameshiriki matembezi ya amani ya kuwahamasisha wakaaziย  kuwa mstari wa mbele katika kuripotiย  visa hivyo punde tuย  vinapototekea katika jamii.

Matembezi hayo yalingโ€™oa nanga katika eneo bunge la shinyalu ambapo yalihusisha wanafunzi wa shule za msingi wakieneza ujumbe kwa umma wa kukomesha dhuluma dhidi ya watoto.

Sharon Ingato aliyeongoza kikosi hiki alisema kwamba dhulumaย  dhidi ya watoto zina madhara mengi kama vile kususia masomo, mimba za mapemaย  na hataย  sehemu za mwili kuharibika kwa mfano watoto wa kiume wanapo lawitiwa .

โ€˜Naomba serikali iweke sheria kali kwa watu watakao patikana kwa makosa yanayohusiana na watoto , pia watoto muwe makini sana mnaporipoti visa hivi maana si kila mtu atakusaidia kupata haki.โ€™ย  Florence Awinoย  adokeza

โ€˜Kila mtoto ana ndoto yake maishani, tunapowadhulumu hawa watoto tunaua ndoto zao maana kuna wale baada ya kitendo hicho hawatarudi shuleni , kuna mwingine atajitoa uhai. Tumejitokeza ili tupiganie haki za watoto na tukomeshe dhuluma dhidi ya watoto katika kaunti hii.โ€™ย  Sharon alieleza.

Matembezi haya yaliungwa mkono na baadhi ya walimu katika eneo hilo na kuwasihi watoto kuwa makini wanaporipoti visa kama hivi maana si kila mtu ni mwaminifu na si wote watahakikisha kwamba haki inapatikana.

โ€˜Naomba serikali iweke sheria kali kwa watu watakao patikana kwa makosa yanayohusiana na watoto , pia watoto muwe makini sana mnaporipoti visa hivi maana si kila mtu atakusaidia kupata haki.โ€™ย  Florence Awinoย  adokeza

Viongozi wa wanaskauti wameionya jamii dhidi ya kushiriki mazungumzo na kutatua visa vya dhuluma nyumbani, wakisema kuwa kwa mara nyingi wahasiriwa hunyimwa haki

โ€˜โ€™Wale wanaotekeleza maovu haya wachukuliwe hatua kali ndiposa idadi yaย  vitendi hivi iweze kurudi chini. Tunaombaย  jamii iwache sheria ichukue mkondo wake, wasiingile kati kwa kutaka kesiย  hizi zisuluhishwe nyumbaniย  hii ndio sababu kubwa ya kuongezeka kwa dhuluma dhidi ya watoto.โ€™โ€™ Sharon alionya.ย  ย 

Mwisho

RELATED ARTICLES

Most Popular

Recent Comments