Saturday, July 27, 2024
spot_img
HomeKenya NewsVisa vya dhuluma dhidi ya watoto vyaongezeka Kakamega

Visa vya dhuluma dhidi ya watoto vyaongezeka Kakamega

Seliphar, Kakamega

Kila siku, kila uchao visa vya dhuluma dhidi ya watoto vinaongezeka katika kaunti ya Kakamega. Ni kipi kinachosababisha visa hizi? Ni hatua gani inayochukuliwa dhidi ya wale wanaotenda unyama huu? Haya ni baadhi tu ya maswali ambayo kupata majibu yake ni muhali.

Hata hivyo wanaskauti  kutoka katika kaunti ya Kakamega  wamejitosa uwanjani kukashifu maovu hayo dhidi ya watoto. Wanaskauti hao  wameshiriki matembezi ya amani ya kuwahamasisha wakaazi  kuwa mstari wa mbele katika kuripoti  visa hivyo punde tu  vinapototekea katika jamii.

Matembezi hayo yaling’oa nanga katika eneo bunge la shinyalu ambapo yalihusisha wanafunzi wa shule za msingi wakieneza ujumbe kwa umma wa kukomesha dhuluma dhidi ya watoto.

Sharon Ingato aliyeongoza kikosi hiki alisema kwamba dhuluma  dhidi ya watoto zina madhara mengi kama vile kususia masomo, mimba za mapema  na hata  sehemu za mwili kuharibika kwa mfano watoto wa kiume wanapo lawitiwa .

‘Naomba serikali iweke sheria kali kwa watu watakao patikana kwa makosa yanayohusiana na watoto , pia watoto muwe makini sana mnaporipoti visa hivi maana si kila mtu atakusaidia kupata haki.’  Florence Awino  adokeza

‘Kila mtoto ana ndoto yake maishani, tunapowadhulumu hawa watoto tunaua ndoto zao maana kuna wale baada ya kitendo hicho hawatarudi shuleni , kuna mwingine atajitoa uhai. Tumejitokeza ili tupiganie haki za watoto na tukomeshe dhuluma dhidi ya watoto katika kaunti hii.’  Sharon alieleza.

Matembezi haya yaliungwa mkono na baadhi ya walimu katika eneo hilo na kuwasihi watoto kuwa makini wanaporipoti visa kama hivi maana si kila mtu ni mwaminifu na si wote watahakikisha kwamba haki inapatikana.

‘Naomba serikali iweke sheria kali kwa watu watakao patikana kwa makosa yanayohusiana na watoto , pia watoto muwe makini sana mnaporipoti visa hivi maana si kila mtu atakusaidia kupata haki.’  Florence Awino  adokeza

Viongozi wa wanaskauti wameionya jamii dhidi ya kushiriki mazungumzo na kutatua visa vya dhuluma nyumbani, wakisema kuwa kwa mara nyingi wahasiriwa hunyimwa haki

‘’Wale wanaotekeleza maovu haya wachukuliwe hatua kali ndiposa idadi ya  vitendi hivi iweze kurudi chini. Tunaomba  jamii iwache sheria ichukue mkondo wake, wasiingile kati kwa kutaka kesi  hizi zisuluhishwe nyumbani  hii ndio sababu kubwa ya kuongezeka kwa dhuluma dhidi ya watoto.’’ Sharon alionya.   

Mwisho

RELATED ARTICLES

Most Popular

Recent Comments