Seliphar, Kakamega
Kila siku, kila uchao visa vya dhuluma dhidi ya watoto vinaongezeka katika kaunti ya Kakamega. Ni kipi kinachosababisha visa hizi? Ni hatua gani inayochukuliwa dhidi ya wale wanaotenda unyama huu? Haya ni baadhi tu ya maswali ambayo kupata majibu yake ni muhali.
Hata hivyo wanaskautiΒ kutoka katika kaunti ya KakamegaΒ wamejitosa uwanjani kukashifu maovu hayo dhidi ya watoto. Wanaskauti haoΒ wameshiriki matembezi ya amani ya kuwahamasisha wakaaziΒ kuwa mstari wa mbele katika kuripotiΒ visa hivyo punde tuΒ vinapototekea katika jamii.
Matembezi hayo yalingβoa nanga katika eneo bunge la shinyalu ambapo yalihusisha wanafunzi wa shule za msingi wakieneza ujumbe kwa umma wa kukomesha dhuluma dhidi ya watoto.
Sharon Ingato aliyeongoza kikosi hiki alisema kwamba dhulumaΒ dhidi ya watoto zina madhara mengi kama vile kususia masomo, mimba za mapemaΒ na hataΒ sehemu za mwili kuharibika kwa mfano watoto wa kiume wanapo lawitiwa .
βNaomba serikali iweke sheria kali kwa watu watakao patikana kwa makosa yanayohusiana na watoto , pia watoto muwe makini sana mnaporipoti visa hivi maana si kila mtu atakusaidia kupata haki.βΒ Florence AwinoΒ adokeza
βKila mtoto ana ndoto yake maishani, tunapowadhulumu hawa watoto tunaua ndoto zao maana kuna wale baada ya kitendo hicho hawatarudi shuleni , kuna mwingine atajitoa uhai. Tumejitokeza ili tupiganie haki za watoto na tukomeshe dhuluma dhidi ya watoto katika kaunti hii.βΒ Sharon alieleza.
Matembezi haya yaliungwa mkono na baadhi ya walimu katika eneo hilo na kuwasihi watoto kuwa makini wanaporipoti visa kama hivi maana si kila mtu ni mwaminifu na si wote watahakikisha kwamba haki inapatikana.
βNaomba serikali iweke sheria kali kwa watu watakao patikana kwa makosa yanayohusiana na watoto , pia watoto muwe makini sana mnaporipoti visa hivi maana si kila mtu atakusaidia kupata haki.βΒ Florence AwinoΒ adokeza
Viongozi wa wanaskauti wameionya jamii dhidi ya kushiriki mazungumzo na kutatua visa vya dhuluma nyumbani, wakisema kuwa kwa mara nyingi wahasiriwa hunyimwa haki
ββWale wanaotekeleza maovu haya wachukuliwe hatua kali ndiposa idadi yaΒ vitendi hivi iweze kurudi chini. TunaombaΒ jamii iwache sheria ichukue mkondo wake, wasiingile kati kwa kutaka kesiΒ hizi zisuluhishwe nyumbaniΒ hii ndio sababu kubwa ya kuongezeka kwa dhuluma dhidi ya watoto.ββ Sharon alionya.Β Β
Mwisho